Moja ya sifa kubwa ya Mtumishi wa Mungu anapaswa kuwa msiri.
__________________________
Neno linasema...
"Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu"
~1cor 4:1
__________________________
Nikiwa katika tafakari ya neno Mungu Roho mtakatifu akanionesha kitu.
wapendwa wengi sio wasiri wa Mungu na ndiyo maana kwa kadri wanavyo endelea kukomaa na tabia Hii Kiwango cha Mungu kuwaamini kinapunguwa na ishara ya kuwa hawaaminiki mbele za Mungu. Mungu huacha au hupunguza kuwapa siri za Mbinguni. kwani kutokuwa msiri ni sawa na kusema umekosa kigezo au sifa cha kuwa mtumishi wa Mungu.
wapendwa wengi ukiwakuta wanaongea utakuta wanamwaga siri za Watu hadharani. kisha hujifariji kwakuambiana ni siri. na kila atakaye sambaza huendelea kusema ni siri. mpaka neno siri linapoteza maana yake.
Mungu kuwaruhusu watu wajekwako mtu wa Mungu waeleza mambo yao ya siri ni kutokana na Mungu kukuamini.
sikumoja Yesu aliwaponya watu kisha akawaambia wasiseme kisha wakasema na kueneza mjimzima.
Neno linasema...
" Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana.Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate. Macho yao yakafumbuka. Naye Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema, Angalieni hata mtu mmoja asijue.Lakini wakatoka, wakaeneza habari zake katika nchi ile yote."
★~Mathayo 9: 28-31
Kumbe ukioneshwa na Mungu jambo ambalo ni siri usimwambie mtu kaa kimya.
hawajamaa Yesu kawa ponya walikuwa vipofu.
lakini wakashidwa kutenda kama alivyo waamuru kwa nguvu. Kweli kuwa mtumishi wa sio jambo jepesi.
Na ukitaka habari ienee mji mzima waambie ni siri..
#Siri
__________________
Minister: Enoch Joseph
Life word Teaching Ministry
★2017
"It is the Spirit who gives life; the flesh profits nothing. The words that I speak to you are spirit, and they are life." ~John 6:63
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Urithi wa watumishi wa Mungu
URITHI WA WATUMISHI WA MUNGU. ------------------------------------------------------------ Hii wengi hawafahamu lakini leo fahamu japo k...

-
Bwana Yesu asifiwe sana! Leo nataka tujifunze juu ya “Mwongozo wa kutafakari na kuombea ndoto zenye UZINIFU AU UASHERATI ndani yake”....
-
SEMINA YA NENO LA MUNGU UWANJA WA TANGANYIKA PACKERS - DAR ES SALAAM MWL.CHRISTOPHER MWAKASEGE TAREHE 15 OKTOBA 2017 *SIKU YA NA...
-
Ninyi wenye kumkumbusha Bwana Juu ya Mambo yahusuyo, Maisha yenu, Familia zenu, Koo zenu, na Jamii zenu Msiwe na Kimya mpaka atakapo f...
No comments:
Post a Comment