Wednesday, 13 December 2017

Sifa ya Mtumishi wa Mungu.

Moja ya sifa kubwa ya Mtumishi wa Mungu anapaswa kuwa msiri.
__________________________

Neno linasema...

 "Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu"
       ~1cor 4:1
__________________________

Nikiwa katika tafakari ya neno Mungu Roho mtakatifu akanionesha kitu.

wapendwa wengi sio wasiri wa Mungu  na ndiyo maana kwa kadri wanavyo endelea kukomaa na tabia Hii Kiwango cha Mungu kuwaamini kinapunguwa na ishara ya kuwa hawaaminiki mbele za Mungu. Mungu huacha au hupunguza kuwapa siri za Mbinguni. kwani kutokuwa msiri ni sawa na kusema umekosa kigezo au sifa cha kuwa mtumishi wa Mungu.

wapendwa wengi ukiwakuta wanaongea utakuta wanamwaga siri za Watu hadharani. kisha hujifariji kwakuambiana ni siri. na kila atakaye sambaza huendelea kusema ni siri. mpaka neno siri linapoteza maana yake.

Mungu kuwaruhusu watu wajekwako mtu wa Mungu waeleza mambo yao ya siri ni kutokana na Mungu kukuamini.

sikumoja Yesu aliwaponya watu kisha akawaambia wasiseme kisha wakasema na kueneza mjimzima.

Neno linasema...

"  Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana.Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate. Macho yao yakafumbuka. Naye Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema, Angalieni hata mtu mmoja asijue.Lakini wakatoka, wakaeneza habari zake katika nchi ile yote."

            ★~Mathayo 9: 28-31

Kumbe ukioneshwa na Mungu jambo ambalo ni siri usimwambie mtu kaa kimya.

hawajamaa Yesu kawa ponya walikuwa vipofu.
lakini wakashidwa kutenda kama alivyo waamuru kwa nguvu. Kweli kuwa mtumishi wa sio jambo jepesi.

Na ukitaka habari ienee mji mzima waambie ni siri..

#Siri

__________________

     Minister: Enoch Joseph
  Life word Teaching Ministry
           ★2017

No comments:

Post a Comment

Urithi wa watumishi wa Mungu

URITHI WA WATUMISHI WA MUNGU. ------------------------------------------------------------ Hii wengi hawafahamu lakini leo fahamu japo k...