Walio vipofu rohoni wapate kuona na walio viziwi rohoni wapate kusikia.
________________
Neno linasema...
" Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona."
~Isaya 42: 18
Mungu aliweka Macho ya rohoni kwa kila mwanadamu na kazi yake ilikuwa waone rohoni. Macho ya utu wa ndani yapate kuona kwa jinsi ya rohoni. Lakini wengi ni vipofu rohoni na hawajuwi kuwa ni vipofu na haiwasumbui kitu wao kuwa vipofu kwasababu Hawajui kuwa wao ni vipofu. Na ivyo hawaombi Mungu awafunguwe Macho ya Ndani kwa sababu hawajui kuwa wanayaitaji ili wafanikiwe na kupiga hatua vizuri katika maisha ya rohoni na Mwilini.
Watu wengi sana ni viziwi wa rohoni na wachache sana wanajuwa kuwa wao ni viziwi. na kwasababu hawajuwi kuwa ni viziwi hawapati tabu wala kujisumbuwa na kumwomba Mungu wapone wapate kusikia. Na hii ni kwasababu hawajui kwamba hawajui kuwa wao ni viziwi. Na hawajui kwamba kufanikiwa kwao katika eneo lolote la maisha yao hapa duniani wanaitaji imani ambayo huja kwa kusikia.
Umebarikiwa wewe usomaye na kusikia ya kwamba Ni mpango wa Mungu uone na nimpango wa Mungu usikie.
Kwa Jina la Yesu upate kusikia ewe uliye kiziwi.
Kwa Jina la Yesu upate kuona wewe uliye kipofu.
Amen.
Imekuwa.
______________________
Minister: Enoch Joseph
Life word Teaching Ministry
★2017.
Ubarikiwe Sana kwa habari njema!
ReplyDelete